Proverbs 3:1-4

Faida Nyingine Za Hekima

1 aMwanangu, usisahau mafundisho yangu,
bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
2 bkwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako
na kukuletea mafanikio.

3 cUsiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe;
vifunge shingoni mwako,
viandike katika ubao wa moyo wako.
4 dNdipo utapata kibali na jina zuri
mbele za Mungu na mwanadamu.
Copyright information for SwhNEN